1. Mimi ni mtu aliyeona matesoKwa fimbo ya ghadhabu yake.
2. Ameniongoza na kuniendesha katika gizaWala si katika nuru.
3. Hakika juu yangu augeuza mkono wakeMara kwa mara mchana wote.
4. Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu;Ameivunja mifupa yangu.
5. Amejenga boma juu yangu,Na kunizungusha uchungu na uchovu.