14. Manabii wako wameona maono kwa ajili yakoYa ubatili na upumbavuWala hawakufunua uovu wako,Wapate kurudisha kufungwa kwako;Bali wameona mabashiri ya ubatili kwa ajili yakoNa sababu za kuhamishwa.
15. Hao watu wote wapitaoHukupigia makofi;Humzomea binti Yerusalemu,Na kutikisa vichwa vyao;Je! Mji huu ndio ulioitwa, Ukamilifu wa uzuri,Furaha ya dunia yote?
16. Juu yako adui zako woteWamepanua vinywa vyao;Huzomea, husaga meno yao,Husema, Tumemmeza;Hakika siku hii ndiyo tuliyoitazamia;Tumeipata, tumeiona.
17. BWANA ameyatenda aliyoyakusudia; amelitimiza neno lake,Aliloliamuru siku za kale;Ameangusha hata chini,Wala hakuona huruma;Naye amemfurahisha adui juu yako,Ameitukuza pembe ya watesi wako.
18. Mioyo yao ilimlilia Bwana;Ee ukuta wa binti Sayuni!Machozi na yachuruzike kama mtoMchana na usiku;Usijipatie kupumzika;Mboni ya jicho lako isikome.
19. Inuka, ulalamike usiku,Mwanzo wa makesha yake;Mimina moyo wako kama maji usoni pa Bwana;Umwinulie mikono yako;Kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa,Mwanzo wa kila njia kuu.