Neh. 7:5-16 Swahili Union Version (SUV)

5. Mungu wangu akanitia moyoni mwangu, kwamba niwakusanye wakuu na mashehe, na watu, ili wahesabiwe kwa nasaba.Nikakiona kitabu cha vizazi vya hao waliokwea hapo kwanza, nikaona ya kwamba imeandikwa humo;

6. Hawa ndio wana wa wilaya, waliokwea kutoka katika ule uhamisho wa hao waliokuwa wamechukuliwa, ambao Nebukadreza, mfalme wa Babeli, aliwachukua mateka, nao wakarudi Yerusalemu na Yuda, kila mtu mjini kwake;

7. ndio hawa waliokuja pamoja na Zerubabeli, Yoshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu, na Baana. Hii ndiyo hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli;

8. Wana wa Paroshi, elfu mbili mia moja sabini na wawili.

9. Wana wa Shefatia, mia tatu sabini na wawili.

10. Wana wa Ara mia sita hamsini na wawili.

11. Wana wa Pahath-Moabu, wa wana wa Yeshua na Yoabu, elfu mbili mia nane na kumi na wanane.

12. Wana wa Elamu, elfu moja mia mbili hamsini na wanne.

13. Wana wa Zatu, mia nane arobaini na watano.

14. Wana wa Zakai, mia saba na sitini.

15. Wana wa Binui, mia sita arobaini na wanane.

16. Wana wa Bebai, mia sita ishirini na wanane.

Neh. 7