24. Na Pethahia, mwana wa Meshezabeli, wa wana wa Zera, mwana wa Yuda, alikuwa wakili wa mfalme kwa habari ya mambo yote ya watu.
25. Na katika habari za vijiji na mashamba yake; wengine wa wana wa Yuda walikuwa wakikaa Kiriath-arba na vijiji vyake, na katika Diboni na vijiji vyake, na Yekabzeeli na vijiji vyake;
26. na katika Yeshua, na Molada, na Beth-peleti;
27. na Hazar-shuali, na Beer-sheba na vijiji vyake;
28. na katika Siklagi, na Mekona na vijiji vyake;
29. na katika Enrimoni, na Sora, na Yarmuthi;
30. Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, Lakishi na mashamba yake, Azeka na vijiji vyake. Hivyo wakatua toka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.
31. Wana wa Benyamini nao walikuwa wakikaa Geba, na Mikmashi, na Aiya, na Beth-eli na vijiji vyake;
32. Anathothi, Nobu, Anania;
33. Hazori, Rama, Gitaimu;
34. Hadidi, Seboimu, Nebalati;