Neh. 11:24-34 Swahili Union Version (SUV)

24. Na Pethahia, mwana wa Meshezabeli, wa wana wa Zera, mwana wa Yuda, alikuwa wakili wa mfalme kwa habari ya mambo yote ya watu.

25. Na katika habari za vijiji na mashamba yake; wengine wa wana wa Yuda walikuwa wakikaa Kiriath-arba na vijiji vyake, na katika Diboni na vijiji vyake, na Yekabzeeli na vijiji vyake;

26. na katika Yeshua, na Molada, na Beth-peleti;

27. na Hazar-shuali, na Beer-sheba na vijiji vyake;

28. na katika Siklagi, na Mekona na vijiji vyake;

29. na katika Enrimoni, na Sora, na Yarmuthi;

30. Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, Lakishi na mashamba yake, Azeka na vijiji vyake. Hivyo wakatua toka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.

31. Wana wa Benyamini nao walikuwa wakikaa Geba, na Mikmashi, na Aiya, na Beth-eli na vijiji vyake;

32. Anathothi, Nobu, Anania;

33. Hazori, Rama, Gitaimu;

34. Hadidi, Seboimu, Nebalati;

Neh. 11