11. Tena utalewa, utafichwa; tena utatafuta ngome kwa sababu ya adui.
12. Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva kwanza; ikitikisika zaanguka katika kinywa chake alaye.
13. Tazama, watu wako walio ndani yako ni wanawake; malango ya nchi yako yamekuwa wazi kabisa mbele ya adui zako; moto umeteketeza mapingo yako.
14. Teka maji yawe tayari kwa kuzingirwa kwako;Zitie nguvu ngome zako;Ingia katika udongo, yakanyage matope,Itie nguvu tanuru ya kuokea matofali.