23. Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24. Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25. Akasema,Na alaaniwe Kanaani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.
26. Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake.
27. Mungu akamnafisishe Yafethi.Na akae katika hema za Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake.
28. Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.
29. Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.