Mwa. 9:23-28 Swahili Union Version (SUV)

23. Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.

24. Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.

25. Akasema,Na alaaniwe Kanaani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.

26. Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake.

27. Mungu akamnafisishe Yafethi.Na akae katika hema za Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake.

28. Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.

Mwa. 9