19. Hawa watatu walikuwa wana wa Nuhu na kwa hao nchi yote ikaenea watu.
20. Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21. akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22. Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23. Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.