18. Wana wa Nuhu waliotoka katika safina, ni Shemu, na Hamu, na Yafethi; na Hamu ndiye baba wa Kanaani.
19. Hawa watatu walikuwa wana wa Nuhu na kwa hao nchi yote ikaenea watu.
20. Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21. akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22. Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23. Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24. Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25. Akasema,Na alaaniwe Kanaani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.
26. Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake.