Mwa. 50:7-9 Swahili Union Version (SUV)

7. Basi Yusufu akaenda amzike babaye, na watumwa wote wa Farao wakaenda pamoja naye, wazee wa nyumbani mwake, na wazee wote wa nchi ya Misri.

8. Na nyumba yote ya Yusufu, na nduguze, na nyumba ya babaye; wakawaacha watoto wao tu, na kondoo zao, na ng’ombe zao, katika nchi ya Gosheni.

9. Kisha wakaenda pamoja naye wapanda farasi, na magari; wakawa jeshi kubwa sana.

Mwa. 50