Mwa. 5:4-18 Swahili Union Version (SUV)

4. Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.

5. Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa.

6. Sethi akaishi miaka mia na mitano, akamzaa Enoshi.

7. Sethi akaishi baada ya kumzaa Enoshi miaka mia nane na saba, akazaa wana, waume na wake.

8. Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa.

9. Enoshi akaishi miaka tisini, akamzaa Kenani.

10. Enoshi akaishi baada ya kumzaa Kenani miaka mia nane na kumi na mitano, akazaa wana, waume na wake.

11. Siku zote za Enoshi ni miaka mia kenda na mitano, akafa.

12. Kenani akaishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.

13. Kenani akaishi baada ya kumzaa Mahalaleli miaka mia nane na arobaini, akazaa wana, waume na wake.

14. Siku zote za Kenani ni miaka mia kenda na kumi, akafa.

15. Mahalaleli akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.

16. Mahalaleli akaishi baada ya kumzaa Yaredi miaka mia nane na thelathini, akazaa wana, waume na wake.

17. Siku zote za Mahalaleli ni miaka mia nane na tisini na mitano, akafa.

18. Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko.

Mwa. 5