18. Wokovu wako nimeungoja, Ee BWANA.
19. Gadi, jeshi litamsonga,Lakini atawasonga wao mpaka visigino.
20. Asheri, chakula chake kitakuwa kinono,Naye atatoa tunu za kifalme.
21. Naftali ni ayala aliyefunguliwa;Anatoa maneno mazuri.
22. Yusufu ni mti mchanga wenye kuzaa,Mti mchanga wenye kuzaa karibu na chemchemi,Matwi yake yametanda ukutani.