Mwa. 46:10-19 Swahili Union Version (SUV)

10. Na wana wa Simeoni; Yemueli na Yamini, na Ohadi, na Yakini, na Sohari, na Shauli, mwana wa mwanamke Mkanaani.

11. Na wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.

12. Na wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela, na Peresi, na Zera; lakini Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani. Na wana wa Peresi, ni Hesroni, na Hamuli.

13. Na wana wa Isakari; Tola, na Puva, na Yashubu, na Shimroni.

14. Na wana wa Zabuloni; Seredi, na Eloni, na Yaleeli.

15. Hao ndio wana wa Lea, aliomzalia Yakobo katika Padan-aramu, na Dina, binti yake. Nafsi zote za wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.

16. Na wana wa Gadi; Sefoni, na Hagi, na Shuni, na Esboni, na Eri, na Arodi, na Areli.

17. Na wana wa Asheri; Imna, na Ishva, na Ishvi, na Beria, na Sera, umbu lao. Na wana wa Beria ni Heberi, na Malkieli.

18. Hao ndio wana wa Zilpa, ambaye Labani alimpa Lea, binti yake, naye akamzalia Yakobo hao, nafsi kumi na sita.

19. Wana wa Raheli, mkewe Yakobo Yusufu na Benyamini.

Mwa. 46