Mwa. 41:15-18 Swahili Union Version (SUV)

15. Farao akamwambia Yusufu, Nimeota ndoto, wala hakuna awezaye kunifasiria; nami nimesikia habari zako, ya kwamba, usikiapo ndoto, waweza kuifasiri.

16. Yusufu akamjibu Farao, akisema, Si mimi; Mungu atampa Farao majibu ya amani.

17. Farao akamwambia Yusufu, Katika ndoto yangu nalikuwa nikisimama ukingoni mwa mto;

18. na tazama, ng’ombe saba wanatoka mtoni, wanono, wazuri, wakajilisha manyasini.

Mwa. 41