Mwa. 37:5-8 Swahili Union Version (SUV)

5. Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia;

6. akawaambia, Tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoiota.

7. Tazama, sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu.

8. Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake.

Mwa. 37