Mwa. 37:16-19 Swahili Union Version (SUV)

16. Akasema, Nawatafuta ndugu zangu; tafadhali uniambie mahali wanakochunga.

17. Yule mtu akasema, Wametoka hapa, maana niliwasikia wakisema, Twendeni Dothani. Basi Yusufu akawafuata ndugu zake akawakuta huko Dothani.

18. Wakamwona toka mbali, na kabla hajawakaribia, wakafanya shauri juu yake ili wamwue.

19. Wakasemezana wao kwa wao, Tazama, yule bwana wa ndoto anakuja.

Mwa. 37