10. Akawaambia baba yake na ndugu zake; baba yake akamkemea akamwambia, Ni ndoto gani hii uliyoiota? Je! Mimi na mama yako na ndugu zako tutakuja tukusujudie hata nchi?
11. Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili.
12. Ndugu zake wakaenda kuchunga kondoo za baba yao huko Shekemu.