Mwa. 37:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Yakobo akakaa katika nchi aliyosafiri baba yake, katika nchi ya Kanaani.

2. Hivi ndivyo vizazi vya Yakobo. Yusufu, aliyekuwa mwenye miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo pamoja na ndugu zake; naye alikuwa kijana pamoja na wana wa Bilha, na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akamletea baba yao habari zao mbaya.

3. Basi Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe wote, maana ni mwana wa uzee wake, akamfanyia kanzu ndefu.

4. Ndugu zake wakaona ya kuwa baba yao anampenda kuliko ndugu zake wote, wakamchukia, wala hawakuweza kusema naye kwa amani.

5. Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia;

6. akawaambia, Tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoiota.

7. Tazama, sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu.

Mwa. 37