Mwa. 36:8-13 Swahili Union Version (SUV)

8. Esau akakaa katika mlima Seiri, Esau ndiye Edomu.

9. Hivi ni vizazi vya Esau, baba ya Edomu katika mlima Seiri.

10. Haya ndiyo majina ya wana wa Esau; Elifazi, mwana wa Ada mkewe Esau. Reuli, mwana wa Basemathi, mkewe Esau.

11. Na wana wa Elifazi, ni Temani na Omari, na Sefo, na Gatamu, na Kenazi.

12. Na Timna alikuwa suria wa Elifazi, mwana wa Esau; naye akamzalia Elifazi Amaleki. Hao ndio wana wa Ada, mkewe Esau.

13. Na hawa ni wana wa Reueli, Nahathi, na Zera, na Shama na Miza. Hao walikuwa wana wa Basemathi, mkewe Esau.

Mwa. 36