25. Na hawa ni wana wa Ana, Dishoni, na Oholibama, binti Ana.
26. Na hawa ni wana wa Dishoni, Hemdani, na Eshbani, na Ithrani, na Kerani.
27. Na hawa ni wana wa Eseri, Bilhani, na Zaawani, na Akani.
28. Na hawa ni wana wa Dishani, Usi, na Arani.
29. Hawa ndio majumbe waliotoka katika Wahori; jumbe Lotani, jumbe Shobali, jumbe Sibeoni, jumbe Ana,
30. jumbe Dishoni, jumbe Eseri jumbe Dishani. Hao ndio majumbe waliotoka katika Wahori, kwa habari za majumbe yao, katika nchi ya Seiri.
31. Na hawa ndio wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu, kabla ya kumiliki mfalme ye yote juu ya wana wa Israeli.
32. Bela wa Beori alimiliki katika Edomu, na jina la mji wake ni Dinhaba.
33. Akafa Bela, akamiliki Yobabu mwana wa Zera, wa Bosra, badala yake.
34. Akafa Yobabu, akamiliki Hushamu, wa nchi ya Watemani, badala yake.
35. Akafa Hushamu, akamiliki Hadadi wa Bedadi badala yake, naye ndiye aliyepiga Midiani katika nyika ya Moabu, na jina la mji wake ni Avithi.
36. Akafa Hadadi, akamiliki Samla wa Masreka badala yake.
37. Akafa Samla, na Shauli wa Rehobothi, ulio karibu na mto, akamiliki badala yake.
38. Akafa Shauli, akamiliki Baal-hanani, mwana wa Akbori, badala yake.
39. Akafa Baal-hanani, mwana wa Akbori, akamiliki Hadadi badala yake; na jina la mji wake ni Pau; na jina la mkewe ni Mehetabeli, binti Matredi, binti Mezahabu.
40. Na hayo ndiyo majina ya majumbe waliotoka kwa Esau, kufuata jamaa zao, na mahali pao, kwa majina yao. Jumbe Timna, jumbe Alva, jumbe Yethethi,
41. jumbe Oholibama, jumbe Ela, jumbe Pinoni,