21. Basi ile zawadi ikavuka mbele yake, naye mwenyewe akakaa usiku ule kambini.
22. Akaondoka usiku ule akawatwaa wakeze wawili, na vijakazi wake wawili, na wanawe kumi na mmoja, akavuka kivuko cha Yaboki.
23. Akawatwaa, akawavusha mto, akavusha na vyote alivyokuwa navyo.
24. Yakobo akakaa peke yake; na mtu mmoja akashindana naye mweleka hata alfajiri.
25. Naye alipoona ya kuwa hamshindi, alimgusa panapo uvungu wa paja lake; ukateguka uvungu wa paja la Yakobo alipokuwa akishindana naye.
26. Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki.
27. Akamwuliza, Jina lako n’nani? Akasema, Yakobo.
28. Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda.
29. Yakobo akamwuliza, akasema, Niambie, tafadhali, jina lako? Akasema, Kwa nini waniuliza jina langu? Akambariki huko.