20. Lea akasema, Mungu amenipa mahari njema, sasa mume wangu atakaa nami, kwa kuwa nimemzalia wana sita. Akamwita jina lake Zabuloni.
21. Baadaye akazaa binti, akamwita jina lake Dina.
22. Mungu akamkumbuka Raheli; Mungu akamsikia, akamfungua tumbo.
23. Akapata mimba, akazaa mwana, akasema, Mungu ameondoa aibu yangu.
24. Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Bwana aniongeze mwana mwingine.
25. Ikawa Raheli alipomzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, Nipe ruhusa niende kwetu, na kwenye nchi yangu.
26. Nipe wake zangu na watoto wangu, niliokutumikia, niende zangu, maana umejua utumishi wangu niliokutumikia.
27. Labani akamwambia, Iwapo nimeona fadhili machoni pako, kaa, maana nimetambua ya kwamba BWANA amenibariki kwa ajili yako.