18. Lea akasema, Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nimempa mume wangu mjakazi wangu. Akamwita jina lake Isakari.
19. Lea akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa sita.
20. Lea akasema, Mungu amenipa mahari njema, sasa mume wangu atakaa nami, kwa kuwa nimemzalia wana sita. Akamwita jina lake Zabuloni.
21. Baadaye akazaa binti, akamwita jina lake Dina.