Mwa. 26:17-19 Swahili Union Version (SUV)

17. Basi Isaka akatoka huko akapiga kambi katika bonde la Gerari, akakaa huko.

18. Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.

19. Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika.

Mwa. 26