17. Basi Isaka akatoka huko akapiga kambi katika bonde la Gerari, akakaa huko.
18. Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.
19. Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika.