Mwa. 22:18-24 Swahili Union Version (SUV)

18. na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.

19. Basi Ibrahimu akawarudia vijana wake, wakaondoka, wakaenda zao pamoja mpaka Beer-sheba; Ibrahimu akakaa huko Beer-sheba.

20. Ikawa baada ya mambo hayo, Ibrahimu akaambiwa ya kwamba, Tazama, Milka naye amemzalia Nahori ndugu yako wana;

21. Usi, mzaliwa wa kwanza wake, na Buzi nduguye, na Kemueli, baba wa Aramu;

22. na Kesedi, na Hazo, na Pildashi, na Yidlafu, na Bethueli.

23. Bethueli akamzaa Rebeka; hao wanane Milka alimzalia Nahori ndugu wa Ibrahimu.

24. Na suria wake Reuma naye alizaa Teba na Gahamu na Tahashi na Maaka.

Mwa. 22