13. Arfaksadi akaishi baada ya kumzaa Sela miaka mia nne na mitatu, akazaa wana, waume na wake.
14. Sela akaishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15. Sela akaishi baada ya kumzaa Eberi miaka mia nne na mitatu, akazaa wana, waume na wake.
16. Eberi akaishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17. Eberi akaishi baada ya kumzaa Pelegi miaka mia nne na thelathini, akazaa wana, waume na wake.
18. Pelegi akaishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
19. Pelegi akaishi baada ya kumzaa Reu miaka mia mbili na kenda, akazaa wana, waume na wake.
20. Reu akaishi miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
21. Reu akaishi baada ya kumzaa Serugi miaka mia mbili na saba, akazaa wana, waume na wake.
22. Serugi akaishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23. Serugi akaishi baada ya kumzaa Nahori miaka mia mbili, akazaa wana, waume na wake.
24. Nahori akaishi miaka ishirini na kenda, akamzaa Tera.
25. Nahori akaishi baada ya kumzaa Tera miaka mia na kumi na kenda, akazaa wana, waume na wake.