12. Arfaksadi akaishi miaka thelathini na mitano, akamzaa Sela.
13. Arfaksadi akaishi baada ya kumzaa Sela miaka mia nne na mitatu, akazaa wana, waume na wake.
14. Sela akaishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15. Sela akaishi baada ya kumzaa Eberi miaka mia nne na mitatu, akazaa wana, waume na wake.