Mwa. 10:10-18 Swahili Union Version (SUV)

10. Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.

11. Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala;

12. na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa.

13. Misri akazaa Waludi, na Waanami, na Walehabi, na Wanaftuhi,

14. na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti na Wakaftori.

15. Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi,

16. na Myebusi, na Mwamori, na Mgirgashi,

17. na Mhivi, na Mwarki, na Msini,

18. na Mwarvadi, na Msemari, na Mhamathi. Baadaye jamaa za Wakanaani walitawanyikana.

Mwa. 10