Mwa. 10:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Hivi ndivyo vizazi vya wana wa Nuhu, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Na kwao walizaliwa wana wa kiume baada ya gharika.

2. Wana wa Yafethi ni Gomeri, na Magogu, na Madai, na Yavani, na Tubali, na Mesheki, na Tirasi.

3. Na wana wa Gomeri ni Ashkenazi, na Rifathi, na Togama.

4. Na wana wa Yavani ni Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Warodani.

5. Kwa hao nchi za pwani za mataifa ziligawanyikana kuwa nchi zao, kila moja kwa lugha yake, kwa jamaa zao, kufuata mataifa yao.

Mwa. 10