Mwa. 1:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tatu.

14. Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka;

15. tena iwe ndiyo mianga katika anga la mbingu itie nuru juu ya nchi; ikawa hivyo.

16. Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia.

17. Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi

Mwa. 1