25. Lakini makutano walipoondoshwa, aliingia, akamshika mkono; yule kijana akasimama.
26. Zikaenea habari hizi katika nchi ile yote.
27. Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, Uturehemu, Mwana wa Daudi.
28. Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana.
29. Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate.
30. Macho yao yakafumbuka. Naye Yesu akawaagiza kwa nguvu, akisema, Angalieni hata mtu mmoja asijue.