Mt. 9:20-27 Swahili Union Version (SUV)

20. Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.

21. Kwa maana alisema moyoni mwake, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.

22. Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.

23. Yesu alipofika nyumbani kwa yule jumbe, aliona wapiga filimbi, na makutano wakifanya maombolezo,

24. akawaambia, Ondokeni; kwa maana kijana hakufa, amelala tu. Wakamcheka sana.

25. Lakini makutano walipoondoshwa, aliingia, akamshika mkono; yule kijana akasimama.

26. Zikaenea habari hizi katika nchi ile yote.

27. Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, Uturehemu, Mwana wa Daudi.

Mt. 9