Mt. 8:30-32 Swahili Union Version (SUV)

30. Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha.

31. Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe.

32. Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini.

Mt. 8