21. Mwingine katika wanafunzi wake akamwambia, Bwana, nipe ruhusa kwanza, niende nikamzike baba yangu.
22. Lakini Yesu akamwambia, Nifuate; waache wafu wazike wafu wao.
23. Akapanda chomboni, wanafunzi wake wakamfuata.
24. Kukawa msukosuko mkuu baharini, hata chombo kikafunikizwa na mawimbi; naye alikuwa amelala usingizi.
25. Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana, tuokoe, tunaangamia.