Mt. 8:19-26 Swahili Union Version (SUV)

19. Mwandishi mmoja akamwendea, akamwambia, Mwalimu, nitakufuata ko kote uendako.

20. Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota; lakini Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake.

21. Mwingine katika wanafunzi wake akamwambia, Bwana, nipe ruhusa kwanza, niende nikamzike baba yangu.

22. Lakini Yesu akamwambia, Nifuate; waache wafu wazike wafu wao.

23. Akapanda chomboni, wanafunzi wake wakamfuata.

24. Kukawa msukosuko mkuu baharini, hata chombo kikafunikizwa na mawimbi; naye alikuwa amelala usingizi.

25. Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana, tuokoe, tunaangamia.

26. Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa imani haba? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu.

Mt. 8