19. Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba;
20. bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi;
21. kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.
22. Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.