Mt. 6:19-22 Swahili Union Version (SUV)

19. Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba;

20. bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi;

21. kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.

22. Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.

Mt. 6