8. Heri wenye moyo safi;Maana hao watamwona Mungu.
9. Heri wapatanishi;Maana hao wataitwa wana wa Mungu.
10. Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki;Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
11. Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.
12. Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.
13. Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.