Mt. 5:26-32 Swahili Union Version (SUV)

26. Amin, nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho.

27. Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;

28. lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.

29. Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.

30. Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.

31. Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka;

32. lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.

Mt. 5