Mt. 5:25-29 Swahili Union Version (SUV)

25. Patana na mshitaki wako upesi, wakati uwapo pamoja naye njiani; yule mshitaki asije akakupeleka kwa kadhi, na kadhi akakupeleka kwa askari, ukatupwa gerezani.

26. Amin, nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho.

27. Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;

28. lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.

29. Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.

Mt. 5