Mt. 5:1-9 Swahili Union Version (SUV)

1. Naye alipowaona makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia;

2. akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema,

3. Heri walio maskini wa roho;Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

4. Heri wenye huzuni;Maana hao watafarijika.

5. Heri wenye upole;Maana hao watairithi nchi.

6. Heri wenye njaa na kiu ya haki;Maana hao watashibishwa.

7. Heri wenye rehema;Maana hao watapata rehema.

8. Heri wenye moyo safi;Maana hao watamwona Mungu.

9. Heri wapatanishi;Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

Mt. 5