Mt. 5:1-12 Swahili Union Version (SUV)

1. Naye alipowaona makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia;

2. akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema,

3. Heri walio maskini wa roho;Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

4. Heri wenye huzuni;Maana hao watafarijika.

5. Heri wenye upole;Maana hao watairithi nchi.

6. Heri wenye njaa na kiu ya haki;Maana hao watashibishwa.

7. Heri wenye rehema;Maana hao watapata rehema.

8. Heri wenye moyo safi;Maana hao watamwona Mungu.

9. Heri wapatanishi;Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

10. Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki;Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

11. Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.

12. Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.

Mt. 5