Mt. 4:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi.

2. Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa.

3. Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.

4. Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

5. Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu,

6. akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa,Atakuagizia malaika zake;Na mikononi mwao watakuchukua;Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

7. Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

Mt. 4