48. Mara mmoja wao akaenda mbio, akatwaa sifongo, akaijaza siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha.
49. Wale wengine wakasema, Acha; na tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.
50. Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.
51. Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
52. makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;