44. Pia wale wanyang’anyi waliosulibiwa pamoja naye walimshutumu vile vile.
45. Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa.
46. Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
47. Na baadhi yao waliohudhuria, waliposikia, walisema, Huyu anamwita Eliya.
48. Mara mmoja wao akaenda mbio, akatwaa sifongo, akaijaza siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha.