4. Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.
5. Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga.
6. Wakuu wa makuhani wakavitwaa vile vipande vya fedha, wakasema, Si halali kuviweka katika sanduku ya sadaka, kwa kuwa ni kima cha damu.
7. Wakafanya shauri, wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.