Mt. 27:28-34 Swahili Union Version (SUV)

28. Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu.

29. Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!

30. Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani.

31. Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha.

32. Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake.

33. Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa,

34. wakampa kunywa divai iliyochanganyika na nyongo; lakini yeye alipoionja hakutaka kunywa.

Mt. 27