Mt. 27:18-20 Swahili Union Version (SUV)

18. Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda.

19. Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.

20. Nao wakuu wa makuhani na wazee wakawashawishi makutano ili wamtake Baraba, na kumwangamiza Yesu.

Mt. 27