13. Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?
14. Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana.
15. Basi wakati wa siku kuu, liwali desturi yake huwafungulia mkutano mfungwa mmoja waliyemtaka.
16. Basi palikuwa na mfungwa mashuhuri siku zile, aitwaye Baraba.