11. Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, Wewe wasema.
12. Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno.
13. Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?
14. Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana.