Mt. 26:17-25 Swahili Union Version (SUV)

17. Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi wake wakamwendea Yesu, wakamwambia, Ni wapi utakapo tukuandalie uile Pasaka?

18. Akasema, Enendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie, Mwalimu asema, Majira yangu ni karibu; kwako nitafanya Pasaka pamoja na wanafunzi wangu.

19. Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaiandaa Pasaka.

20. Basi kulipokuwa jioni aliketi chakulani pamoja na wale Thenashara.

21. Nao walipokuwa wakila, alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu atanisaliti.

22. Wakahuzunika sana, wakaanza kumwuliza mmoja mmoja, Ni mimi, Bwana?

23. Akajibu akasema, Yeye aliyetia mkono wake pamoja nami katika kombe, ndiye atakayenisaliti.

24. Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa.

25. Yuda, yule mwenye kumsaliti, akajibu, akasema, Ni mimi, Rabi? Akamwambia, Wewe umesema.

Mt. 26